
Tukio hilo lilichukua nafasi wikiendi iliyopita kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini lililofanyika katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar ambapo mwanadada huyo aliambatana na mashosti zake kushuhudia burudani tofauti ikiwemo mechi ya timu ya Bongo Fleva na Movies anayoichezea mpenzi wake.
Chuchu alivaa t-shirt ya njano ambayo mgongoni ilikuwa imeandikwa Ray Kigosi kitu ambacho hakuwahi kukifanya kabla.“Sioni tatizo kujinadi hadharani, atakayemaindi shauri yake, nafanya kitu roho inapenda bwana sijali maneno ya watu hata kidogo,” alifunguka Chuchu.usiku wa matumaini 2014..
Sign up here with your email