SUMU YA PENZI: MPENZI WAKO AKIKUAMBIA MANENO HAYA, ZINDUKA!

UNAWEZA kuambiwa maneno mengi sana kutoka kwa mpenzi wako, mazuri na mabaya lakini yapo ambayo yanatoa taswira isiyo nzuri. Jambo la msingi ni kuwa makini kupambanua.Pointi ya msingi hapa ni lugha zenye ishara mbaya kwa wapenzi. Umewahi kujiuliza kuhusu hili? Umewahi kutafakari juu ya kauli chafu anazotoa mpenzi wako dhidi yako?Kauli za maudhi, kashfa na hata matusi wakati mwingine, wewe unazichukuliaje? Rafiki zangu, kauli ya mtu inaw eza kukutoa gizani na kugundua ukweli uliopo ndani yake, lakinikama hutakuwa makini, unaweza kuchukulia kama utani na kuuacha ukweli uendelee, mwisho unakuja kushtuka, umeshaachwa!Hapa nimekuandalia kauli zenye ishara mbaya ya penzi lako. Ukiona moja kati ya kauli zifuatazo, basi kuwa na mashaka, kisha fanyia kazi, utagundua ukweli.AKIKUAMBIA HUVUTII!Kati ya kauli mbaya zaidi katikauhusiano ni pale mpenzi wako atakapokuambia huna mvuto! Haijalishi amekuambia akiwa katika hali gani; utani au akimaanisha, lakini neno hilo si zuri kuambiwa na mpenzi wako.Kuambiwa huvutii, katikamapenzi ni tusi kubwa. Nini maana ya mvuto basi? Nani umvutie? Ni wapita njia? Ofisini? Sokoni? Ana maana gani?Siku zote mvuto ni kwa ajili ya mpenzi wako, ndiyo maana mkawa katika uhusiano, hii inamaanisha ulimvutia ndiyo sababu akakukubali. Kukuambia huvutii si utani, ni kweli haoni mvuto na inawezekana penzi limeshachuja.Inawezekana akawa anafanya mzaha, kama ndivyo, atasoma ulivyopokea, akiona umekasirika atarekebisha usemi wake haraka, kama ni vinginevyo ataendelea kushikilia msimamo wake, hata kama ni kwa utani, lakini atakuwa anakufikishia ujumbe wako kwamba huna mvuto, kwa maneno mengine humvutii, humfai; kwa hiyo muachane. Kuna nini tena hapo? Akili kichwani mwako.Hii ni kauli nyingine mbaya. Unapoambiwa: “Hujapendeza kabisa, yaani huna uwezo wa kupangilia nguo, kila siku unachemsha!” Ujue kuna hatari hapo, angalia mara mbiliuhusiano wenu.Kuambiwa hujapendeza kunashusha thamani yako na kuonekana huna ujanja wa kufanya uchaguzi mzuri wa mavazi. Huenda ni kweli hujapendeza, lakini hilo si la kubeza.Anatakiwa kukuambia kwa upole namna ambavyo unatakiwa kuvaa na kuonekana nadhifu. Kwa maneno mengine, kukuambia hujapendeza ni kama anakusuta, hakukubali na unamuaibisha
Previous
Next Post »

Blogger templates