Ama kweli uswazi hakuishi vijimambo! Mganga wa jadi almaarufu sangoma aliyetajwa kwa jina la Wadebi Jinasa amepata aibu ya karne baada ya kunaswa ‘live’ na wake za watu kwenye gesti moja (jina linahifadhiwa) iliyopo Tandika jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo la aina yake lilijiri maeneo hayo, usiku wa manane wa kuamkia Jumanne iliyopita, wakati waumini wa Dini ya Kiislamu waliofunga kwa ajili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani wakila daku.
Kwa mujibu wa mashuhuda, jamaa huyo alidaiwa kuwa alikuwa akiwafanyia wake hao wa watu dawa ya mapenzi kwa kuwavua nguo zote kisha ‘kuwachezea’.
Ilidaiwa kuwa mbali na kuwachezea, amekuwa akiwafanyia mchezo usiofaa mmoja baada ya mwingine.Chanzo cha sakata hilo kilidai kuwa sangoma huyo amekuwa na tabia hiyo hasa akimuona mwanamke mwenye mvuto katika hali ambayo haikueleweka mara moja humuita majina yake matatu, yaani la kwake, baba hadi la babu yake, jambo linalosababisha anayeitwa kushtuka na kuhisi mtu huyo atakuwa anamfahamu kiundani.
Ilidaiwa kuwa baada ya mwanamke huyo kusimama huanza kumwelezea matatizo yake na kumtajiwa hadi matatizo yanayowapata ndugu zake walio vijijini na sehemu nyingine za mbali.
Kiliendelea kudai kwamba, sangoma huyo amekuwa akiwavuta wanawake wengi kwa kuwatajia matatizo yao sawia bila kukosea hivyo kuwachanganya na kumjengea imani kuwa ni ‘fundi’ wa masuala hayo.
Baada ya mke wa Huruka kuokolewa kufanyiwa ukenge, mwanamke mwingine wa eneo hilo, Tabu Abdallah naye alidai kumnasa mkewe kwenye gesti hiyo akiwa amekalishwa kama alivyozaliwa, akitolewa vitu fulani tumboni na sangoma huyo.
Akizungumza na Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publisher ambayo ilifika eneo hilo usiku baada ya kutonywa na chanzo chake, Tabu alisema alimnasa mkewe na sangoma huyo baada ya kutonywa juu ya mkewe kuingia gesti hiyo.
Alisema sangoma huyo alimchukua mkewe kwa gia ya kumtibia kumbe alikuwa na lake jambo.
Baada ya kutokea kwa mtiti huo, Mjumbe wa Shina namba 29, Azimio-Tandika, Faraj Neto, wanawake waliodhalilishwa, waume zao, polisi na mmliki wa gesti hiyo, Ebenezer Ngowo, walimchomoa sangoma huyo kwenye gesti hiyo.
Katika hali ya kushangaza mke wa Tabu alikuwa akimlaumu mumewe kwa kutaka kumpiga mganga wake ambaye alikuwa akitaka kummalizia matatizo huku wanawake wengine wakiwaomba radhi waume zao na kudai walirubuniwa.
Akizungumizia mkasa huo mke wa Tabu alisema kuna siku alikutana na mganga huyo njiani ambapo alimwita majina yake matatu, aliposimama kumsikiliza ndiyo akaanza kumtajia matatizo yake, jina la mama yake mzazi na kumwambia mama huyo huko aliko ana tatizo sugu la miguu jambo ambalo ni kweli ndipo alianza kumuamini.
MWISHO WA SAKATA
Mwisho wa sakata hilo, mjumbe wa nyumba kumi alimtaka sangoma huyo kuondoka eneo hilo na mmiliki wa gesti hiyo alimtaka mganga huyo kuhama kwenye gesti yake kutokana na tabia yake ya kubadilisha wanawake.
Kwa upande wao, polisi walimshikilia sangoma huyo kutokana na sababu za kiusalama kufuatia wenye wake na wananchi wenye hasira kutaka kumpiga mawe na kumuua.
MWISHO WA SAKATA
Mwisho wa sakata hilo, mjumbe wa nyumba kumi alimtaka sangoma huyo kuondoka eneo hilo na mmiliki wa gesti hiyo alimtaka mganga huyo kuhama kwenye gesti yake kutokana na tabia yake ya kubadilisha wanawake.
Kwa upande wao, polisi walimshikilia sangoma huyo kutokana na sababu za kiusalama kufuatia wenye wake na wananchi wenye hasira kutaka kumpiga mawe na kumuua.
Sign up here with your email