wasanii
LULU Afunguka juu ya tetesi za kupata Mchumba..!!
LULU Afunguka juu ya tetesi za kupata Mchumba..!!
BINTI anayeshikilia Tuzo ya Mwigizaji Bora wa Kike ya
Ziff 2013, Elizabeth Michael maarufu Lulu ameweka wazi kuwa amepata
mchumba na kwamba taratibu za kujitambulisha na mahari vitafuata
baadaye.“Unajua mimi ni binadamu na ili nitulie na kujiepusha na
majanga, ni vyema kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu, anayenijali mimi na
kazi yangu hapo nitasimama na kusema kwamba nimepata sehemu ya kutulia
na kuanza maisha mapya ya uhusiano na ndoa,” anasema Lulu.Hata hivyo anasema yeye na mchumba huyo (ambaye hakutaka
kuweka wazi jina lake) wana mikakati mingi katika kuyafikia maisha ya
uhusiano yaliyo wazi na yenye baraka za wazazi.“Siwezi kukutajia jina kwa sasa itafika wakati atajulikana
tu, hata hivyo bado hatujafikia hatua muhimu ikiwa ni pamoja na
kujitambulisha kwa wazazi na masuala ya mahari na ndoa. Vitu kama hivi
vitafanyika baadaye mwaka huu, hata hivyo wazazi wangu sidhani kama
watakuwa na pingamizi katika hili kwani mimi ni mtoto wa kike na nimekua
sasa,” anasema.Kuhusu Mama Kanumba Lulu anasema: “Huyu ni mama yangu hana
tofauti na mama Lulu hivyo anajua kila kitu na amenipa baraka zake zote,
yaliyopita si ndwele kinachotakiwa ni kuganga yajayo, namshukuru mama
kwani amenionyesha upendo wa kweli na kunishauri katika maisha, bila
yeye nisingekuwa na ujasiri nilionao sasa. “Mama Kanumba ni rafiki yangu wa ukweli, ana mapenzi mazito
sana kwangu amekuwa mstari wa mbele kunishauri na kunipa mwongozo wa
maisha ni nini na wapi nilipokosea na natakiwa kufanya nini ili kuwa na
maisha yaliyonyooka,” anasema mwigizaji huyo anayetamba na filamu ya
Foolish Age.Lulu mwenye miaka 19, anasema haikuwa rahisi kwake kufikiria
kutulia kiuhusiano ila amepewa mwongozo bora unaomfanya afikirie
kufanya hivyo kwa sasa.“Mimi ni binti na kama ujuavyo nina mapenzi yangu moyoni, si
kazi rahisi kuamua kwa sasa lakini nimepewa mwongozo bora na kuona nini
natakiwa kufanya. Kama binti napaswa kuzingatia maadili, mimi ni kioo
cha jamii, inafika hatua inabidi niishi katika maadili hilo ndilo
ninalolifanya sasa.”Anasema wazazi wake wamempa baraka zote kuhusu uhusiano wake
wa sasa: “Wazazi wangu sasa wanafahamu kwamba nimepata mchumba, kwa
kweli wamenipa baraka zao zote, pande zote hata Mama Kanumba. Nimekua
sasa na mimi nina uamuzi wangu, ni vema kuangalia ninataka nini lakini
kikubwa wananishauri.”Anasema wazazi wake hawakubali kila anachokitaka: “Sina
wazazi wa kukubali kila ninachokitaka ila nina wazazi waelewa, wenye
kuangalia jambo kabla hawajaniambia sasa unaweza kuendelea, mama yangu
ni mkali sana, hana mchezo hasa pale anapoona kwamba nayumba kimaisha,”
anasema Lulu.Kuhusu tetesi zilizoenea kwamba ana uhusiano na msanii wa
hip hop Young Dee, Lulu alikana na kusisitiza kwamba hajawahi hata kuwa
na ukaribu na msanii huyo.“Nashangaa taarifa hizo watu wanazitoa wapi na mpaka leo
nashangazwa na uvumi ulioenea kwamba tulifumaniwa, usiku ule nilikuwa
sehemu nyingine tofauti kabisa, ukweli ni kwamba sijawahi kuwa na
ukaribu na Young Dee, wala hata kumfikiria kama ninaweza kuwa na
uhusiano naye. Bado, hatulingani kwa kweli,” anasema.