Kioja…Avunja Ndoa yake kwa kutamani maisha ya Wema Sepetu..!

Kuiga  ni  kawaida  kwa  wengi.Wapo  walioiga  mambo  fulani  na   hatimaye  wakafanikiwa, na  pia  wapo  walioiga  vitu  flani  wakaharibikiwa.Huyu  aliiga  na  akaharibu  kila  kitu…
Ni  msanii  wa  siku  nyingi  katika  fani.Alitamba  zaidi  akiwa  Kaole, na  hata  mwanzoni  mwa  ujio  wa  filamu  za  Kanumba  alizidi  tu  kashaini….
Kiasili  ni  mweusi  japo  siku  hizi  kuna  weupe  fulani  katika  ngozi  yake  nyororo.Ana  sura  nzuri  yenye  mvuto,umbo  aslia  la  kibantu,meno  yake  meupe  yamepambwa  na  mwanya  mdogo  na  kufanya  iwe  fahari  kumuona  akitabasamu…
Wema Sepetu ‘Madam’.
Wema Sepetu ‘Madam’.
Hana  kashfa  ya  kuvaa  nguo  fupi  sana  ila  aliwahi  kukumbwa  na  skendo  kubwa  zaidi.Mkumbuke  vizuri.Mrefu  wa  wastani,anajua  kutembea,anaongea  kwa  mapozi  huku  akipenda  kulamba  papi  ya  midomo  yake.Umemjua???….Hapana, siyo  huyo…!!
Huyu  ni  mpole  kiasili  na  anapendwa  sana  na  mama  yake.Katika  maigizo  ana  uwezo  wa  kukufanya  uamini  unachoangalia  ni  kitu  halisi.Japo  huwezi  kumtaja, ila  ndani  ya  wasanii  kumi  anapaswa  kuwamo…
Na  ingawa  mvuto  wake  umepungua  kiasi,ila  bado  mrembo  sana.Lakini  wakati  anaigiza  Kaole  alikuwa  mrembo  zaidi.Kwa  uzuri  wake ,  alivuma  na  kila  habari  inayohusu  mwanaume  maarufu  na  mwenye  pesa
Habari  ya  kutakiwa  na  kila  mwanaume , wenye  rangi  na    vipato  tofauti  zilisikika  kila  kona.Baadhi  alitoka  nao  na  wengine  haikuwa  bahati  yao….
Toka  kitambo  almanusura  aolewe, ila  ni  miaka  ya  juzi juzi  ndipo  aliolewa.Uzuri  wake  si  wa  kutafuta, kila  mwenye  macho  na  ngozi  ya  kuhisi  atautambua….
Mbali  na  majanga  yote  aliyopitia  katika  maisha  yake,mengine  yakibaki  kumchafua  na  watu  kudhani  hawezi  kuolewa  na  mwanaume  yeyote  kabla  ya  ile  bahati  ya  mtende  akaolewa; yeye  aliamua  kuachana  na  ndoa  yake  kwa  kuona  aishi  katika  umaarufu  wake….
Mara  kadhaa  alikuwa  akiwaambia marafiki  zake  kuwa, mwenye  hadhi  na  anayetakiwa  kuishi  kama  Wema  Sepetu  sio  Wema  bali  ni  yeye  na  wakongwe wengine  waliosotea  sanaa  na  kuipigania  kama  roho  zao  na  kuilinda  kama  mboni  ya  jicho  lao…..
Akaona  ndoa  sio  mahala  pake,bila  sababu  za  msngi  akaamua  kumwambia  mumewe  watengane….Japo  haikuwa  rahisi ,lakini  walitengana!!
Cha  kufurahisha  ni  kwamba  bado  Wema  anaishi  kama  Wema  na  bado  yeye  haishi  kama  Wema  Sepetu  na  ndoa  haipo  tena…Umemjua  ninayemzungumzia?
Previous
Next Post »

Blogger templates