Mbali na wageni waalikwa, Lowasa alijumuika na familia yake akiwemo mkewe, Regina Lowassa ambaye pia alionekana akiambatana na mumewe kwa kuwasalimia ndugu wageni waalikwa.
Waalikwa walimuomba Mh Lowassa kujenga utaratibu huo kila mwaka, ili kudumisha umoja na mshikamano.
Waalikwa katika shughuli hiyo, walikuwa ni pamoja na maaskofu na viongozi wengine wa dini wa ndani na nje ya nchi.
Waalikwa hao walimpongeza Mh Lowassa kwa kitendo cha kuamua kujumuika pamoja na ndugu zake na viongozi mbalimbali kwani kimeonesha ishara ya upendo.
“Ni jambo zuri sana Mh Lowassa amefanya kwa ndugu zake. Mwaka mpya ndiyo huu unaanza hivyo si vibaya akikutana na kufurahi pamoja na wadau mbalimbali,” alisema mmoja wa waalikwa.
Sign up here with your email